Afrika Kusini yashirikisha vikosi vya usalama kukabiliana na magenge

Ramaphosa aagiza jeshi kushirikiana na polisi

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa ametangaza kuwa jeshi litashirikiana na polisi ili kupambana na viwango vya juu vya uhalifu wa magenge nchini humo. Katika hotuba yake ya kila mwaka kwa taifa, Ramaphosa alieleza kuwa karibu watu 60 wanauawa kila siku, hususan kutokana na vita vya magenge ya dawa za kulevya mjini Cape Town na ufyatulianaji risasi unaohusiana na uchimbaji haramu wa madini jijini Johannesburg.

Ameagiza wakuu wa polisi na jeshi kuandaa mpangokazi wa kupeleka vikosi vya usalama katika mikoa ya Western Cape na Gauteng ndani ya siku chache zijazo. Hatua nyingine ni pamoja na kuajiri maafisa wapya wa polisi 5,500 na kuimarisha ukusanyaji wa taarifa za kijasusi ili kutambua makundi ya uhalifu.

Ramaphosa alisisitiza kuwa uhalifu wa magenge ni tishio kubwa kwa demokrasia, jamii na uchumi wa taifa, akiongeza kuwa athari zake hupimwa kwa maisha yanayopotea, hofu inayotanda katika jamii na kusitasita kwa wawekezaji kuwekeza nchini.

CHANZO: Newstimehub

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#