Rais wa Marekani amesema ni 'aibu' kwa Herzog kwa kutotoa msamaha, huku ofisi ya rais wa Israel ikisema ombi hilo linafanyiwa tathmini.

Trump amlaumu rais wa Israel kwa kutotoa msamaha kwa Netanyahu

Rais wa Marekani Donald Trump amesema Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu sharti apate msamaha katika kesi yake ya ufisadi, na kusema kuwa Rais wa Israel Isaac Herzog sharti aone "aibu" kwa kutotoa msamaha.

Akizungumza katika ikulu ya White House Alhamisi, Trump amesema Netanyahu amekuwa "waziri mkuu bora katika kipindi cha vita" na kwamba raia wa Israel sharti wamdhalilishe Herzog kwa kutotoa msamaha.

"Anatia aibu kwa kutotoa. Sharti atoe," Trump alisema.

Netanyahu alikutana na Trump mjini Washington Jumatano kwa ajili ya mazungumzo kuhusu mpango wa nuklia wa Iran.

Huu ni mkutano wa saba kati yao tangu Trump kuingia madarakani.

Rais akana madai

Netanyahu ni Waziri Mkuu wa kwanza ambae yuko madarakani kushtakiwa.

Trump amemtaka Herzog mara kadhaa kumsamehe Netanyahu na alisema mwezi Disemba kwamba ameambiwa na Herzog kwamba msamaha huo utafanyika punde.

Hata hivyo, ofisi ya Herzog ilikana taarifa hizo.

Katika kujibu kauli ya hivi karibuni ya Trump, ofisi ya rais wa Israel imesema ombi hilo linafanyiwa tathmini na litazingatiwa bila ushawishi kutoka nje wala ndani.

Kwa mujibu wa Sheria ya Israel, ni rais peke ndio mwenye mamlaka ya kutoa msamaha.

Hata hivyo, hakuna msamaha uliotolewa wakati kesi inaendelea.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#