Wametaka kuwepo kwa kanuni madhubuti, ufuatiliaji huru na uwajibikaji zaidi kutoka kwa makampuni ya madini na serikali zinazotoa leseni.

Wataka uwajibikaji kwa familia zilizoathirika migodini

Wanaharakati wa mazingira chini ya bendera yao ya 'Indaba Mbadala ya Madini' waliandamana nje ya mkutano mkuu wa madini maarufu Indaba ya Madini huko Cape Town nchini Afrika Kusini.

Maandamano hayo yalifanyika Februari 11, 2026, ambapo wamezitaka serikali na makampuni ya uchimbaji madini kuchukua hatua zaidi ili kulinda jamii zilizoathirika na uchimbaji wa madini.

Kundi hilo lilisema kuwa mkutano huo wa kila mwaka wa wadau wa madini na wawekezaji unaendelea kupuuza hasara za kimazingira na jamii zinazoathiriwa na shughuli zao kote barani Afrika.

Wakati huo huo, walitaka kuwepo kwa kanuni madhubuti, ufuatiliaji huru na uwajibikaji zaidi kutoka kwa makampuni ya madini na serikali zinazotoa leseni.

Indaba ya Madini ni moja ya mikusanyiko mikubwa ya sekta ya madini barani Afrika, inayovutia wawekezaji wa kimataifa, wakati Indaba Mbadala ya Madini inajiweka kama jukwaa linalowakilisha sauti za wananchi.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#