Sport
Dollar
41,2959
0.01 %Euro
48,7616
0.31 %Gram Gold
4.903,4200
0.38 %Quarter Gold
0,0000
%Silver
0,0000
%Kiongozi wa upinzani nchini Uganda wa chama cha PFF, Kizza Besigye, tangu awekwe kizuizini hivi sasa zimetimia siku 300. Besigye anashikiliwa kwa madai ya kumiliki silaha kinyume cha sheria pamoja na uhaini.
Katika hatua kubwa ya kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2026, chama cha upinzani cha People’s Front for Freedom (PFF), kinachohusishwa na mwanasiasa mkongwe wa upinzani Kizza Besigye, kimetangaza rasmi kuwa hakitatoa mgombea urais katika uchaguzi ujao.
Tangazo hilo lilitolewa na viongozi wa PFF katika mkutano na waandishi wa habari, likieleza kuwa hatua hiyo inalenga kusaidia juhudi za upinzani kuungana na kuondoa utawala wa muda mrefu wa Rais Yoweri Museveni kwa njia ya mshikamano badala ya kugawanyika kwa wagombea wengi.
“Tumeamua kutotoa mgombea Urais mwaka 2026. Lengo letu ni kuhakikisha kuna mgombea mmoja wa upinzani kwa pamoja,” alisema Ibrahim Ssemuju Nganda, Katibu Mkuu wa chama cha PFF.
Wito wa umoja wa vyama vya upinzani
PFF tayari imesaini makubaliano ya ushirikiano na chama cha Alliance for National Transformation (ANT) kinachoongozwa na Jenerali mstaafu Mugisha Muntu, mwezi Julai 2025.
Mazungumzo pia yanaendelea kati ya PFF na chama cha National Unity Platform (NUP) kinachoongozwa na Robert Kyagulanyi, maarufu kama Bobi Wine, kwa lengo la kupata mgombea mmoja kutoka upinzani kuelekea uchaguzi wa 2026.
Comments
No comments Yet
Comment