Sport
Dollar
41,3013
-0.14 %Euro
48,5993
0.04 %Gram Gold
4.834,9600
-0.22 %Quarter Gold
0,0000
%Silver
0,0000
%Makamu huyo wa Kwanza wa Rais wa Sudan Kusini Riek Machar ameshtakiwa kwa mauaji, uhaini na uhalifu dhidi ya binadamu.
Timu ya utetezi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan Sudan_Kusini, Riek Machar, na washtakiwa wengine saba imesema iko tayari kwa kesi itakayowakilishwa.
“Septemba 12, sisi kama timu ya wanasheria ya Riek K Machar tulimtembelea alipo kizuizini. Hii ilikuwa mara ya kwanza yeye kutembelewa tangu 26 machi 2025 alipokamatwa na kuwekwa kizuizini nyumbani,” timu hiyo ilisema katika taarifa iliyoandikwa na Kur and Co Advocates, kwa niaba ya timu yake ya mawakili.
“Tunaangalia hii kama msingi muafaka wa kuhakikisha haki katika kesi na kulinda haki za mtuhumiwa kuwasiliana na baraza lake la sheria,” taarifa iliongezea.
Makamu huyo wa Kwanza wa Rais wa Sudan Kusini Riek Machar ameshtakiwa kwa mauaji, uhaini na uhalifu dhidi ya binadamu.
Waziri wa Sheria nchini humo alisema kuwa Machar alihusika katika mashambulizi ya wanamgambo wa kikabila dhidi ya vikosi vya serikali mwezi Machi.
Machar amekuwa katika kizuizi cha nyumbani tangu mwezi Machi kuhusiana na mashambulizi ya wanamgambo maarufu" white army" ambao walishambulia mji wa kaskazini mashariki wa Nasir, mwezi Machi.
Comments
No comments Yet
Comment