Hata hivyo, hapakuwa na taarifa yoyote kuhusu jambo hilo kutoka kambi ya AFC/M23.

Serikali ya DRC yakubali kumaliza mapigano na waasi wa M23

Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imekubaliana na pendekezo la Angola la kumaliza mapigano yake na kikundi cha waasi wa M23.

Hayo yanajiri kufuatia kikao cha hivi karibuni kilichoketi jijini Luanda, baina ya  Rais wa DRC Felix Tshisekedi, Joao Lourenco wa Angola na Faure Gnassingbe wa Togo.

Wengine walioshiriki kikao hicho ni pamoja na rais wa zamani wa Nigeria, Olusegun Obasanjo, ambaye ni mmoja ya wawezeshaji wa mchakato wa upatikanaji amani nchini DRC.

Hata hivyo, hapakuwa na taarifa yoyote kuhusu jambo hilo kutoka kambi ya AFC/M23.

Tangu Januari 27 mapigano yanaendelea katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kivu Kusini huku waasi wa M23 wakiteka maeneo, na kulazimisha raia kuhamia kwenye kambi za wakimbizi wa ndani.

Rasimu ya azimio la Umoja wa Mataifa iliyosambazwa kabla ya kikao inalaani msaada wa kijeshi wa Rwanda kwa M23 na inazitaka pande zote kusitisha uhasama na kuruhusu misaada ya kibinadamu kufika kwa waathiriwa.

 

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#