Tukio hilo lilihudhuriwa na Rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine na Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius jijini Munich.

Ukraine yapokea shehena ya droni za kivita kutoka Ujerumani

Ukraine imepokea shehena ya kwanza ya droni za kijeshi kama sehemu ya ushirikiano wa kiulinzi kati yake na Ujerumani.

Tukio hilo lilihudhuriwa na Rais Volodymyr Zelenskyy wa Ukraine na Waziri wa Ulinzi wa Ujerumani Boris Pistorius jijini Munich, siku ya Ijumaa.

"Miezi michache iliyopita, tulikubaliana kushirikiana katika eneo la ulinzi, na tumeweza kuikabidhi Ukraine shehena ya kwanza ya droni zilizotengenezwa Ujerumani,” alisema Pistorius.

Kulingana na Pistorius, droni hizo zitakabidhiwa kwa majeshi ya ulinzi ya Ukraine.

Pistorius aliongeza kuwa, nchi hiyo imeweka shabaha ya kutengeneza droni 10,000 ifikapo mwisho wa mwaka 2026.

"Vifaa hivi hutumika wakati wa mapambano, ujasusi na wakati wa kutoa msaada kwenye uwanja wa vita," aliongeza.

Kwa upande, Rais Zelenskyy, ambaye yupo nchini Ujerumani kwa ajili ya Mkutano wa Usalama unaofanyika jijini Munich, aliishukuru serikali ya Ujerumani kwa msaada huo, akiahidi kuiunga mkono nchi hiyo katika miradi yake mbalimbali barani Ulaya.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#