Hatua hiyo, inafuatia malalamiko yaliyoibuliwa na kikundi cha wanasheria wa Israel cha nchini Uingereza.

Makumbusho ya Uingereza yaondoa neno ‘Palestina’ kwenye kuta zake

Makumbusho moja nchini Uingereza imeondoa nene Palestina kutoka kwenye moja ya maonesho yake ya ndani yenye kuhusu historia ya kale ya Mashariki ya Kati.

Hatua hiyo, inafuatia malalamiko yaliyoibuliwa na kikundi cha wanasheria wa Israel cha nchini Uingereza.

“Makumbusho hiyo inapitia upya baadhi ya picha na machapisho ya kwenye kuta zake baada ya kubainika kuwa, matumizi ya neni Palestina hayana umuhimu tena," walisema wanasheria hao siku ya Jumamosi.

Aidha, wanasheria hao walidai kuwa kulikuwa kuna na “kasoro za kihistoria” kuhusu Palestina kwenye machapisho na maonesho hayo.

Kulingana na wanasheria hao, matumizi ya neno hilo yangefuta mabadiliko ya kihistoria yaliyojitokeza.

Wanasheria hao, walidai katika taarifa yao kuwa, makumbusho hiyo ilikuwa kwenye mchakato wa kusasisha machapisho na picha zilizomo kwenye kuta zake.

 

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#