Mvua hizo zimemaliza hali ya miaka saba ya kiangazi.

Wakazi wa Morocco warejea katika mji uliokumbwa na mafuriko

Mamlaka nchini Morocco zimeanza kuandaa mpango wa kurejesha pole pole wakazi wa mji wa Ksar El Kebir na maeneo mengine ya kaskazini magharibi ambapo hali ya hewa imeimarika, shirika la habari la serikali limesema siku ya Jumatatu.

Mamlaka zikisaidiwa na jeshi zimefanikiwa kurudisha watu 188,000 tangu mwanzoni mwa mwezi Februari, ili kuwalinda kutokana na mito iliopasua kingo zake na kusomba ekari 110,000 kaskazini magharibi.

Wakazi wengi wa Ksar El Kebir, kilomita 213 kaskazini mwa mji wa Rabat, sasa wameruhusiwa kurudi katika nyumba zao, isipokuwa wale wa mitaa michache, wizara ya mambo ya ndani ilisema Jumatatu.

Kuimarisha miundombinu

Morocco ina mpango wa kutumia dirham bilioni 3 (dola milioni $330) kuimarisha miundombinu na kuwasaidia wakazi wa maeneo yaliyokumbwa na mafuriko, wakulima, na wamiliki wa maduka katika maeneo ya mafuriko, ofisi ya waziri mkuu ilisema wiki iliopita.

Bwawa na Oued Makhazine, ambalo limefika uwezo wa asilimia ya 160, limelazimika kufungulia maji baada ya kufurika, kutokana na maji kujaa kwenye mto Loukous.

Mvua katika msimu huu wa baridi ilikuwa kwa kiwango cha asilimia 35 ikiwa ni zaidi ya wastani uliotarajiwa tangu miaka 90 na mara tatu zaidi kuliko mwaka uliopita, twkwimu rasmi zimeonesha.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#