Mkutano wa siku mbili Addis Ababa watangaza utumwa na ukoloni kuwa mauaji ya kimbari na uhalifu dhidi ya Waafrika.

Viongozi wa Umoja wa Afrika Wapitisha Azimio Kuhusu Utumwa na Ukoloni

Viongozi wa umoja wa Afrilka waliokutana katika mkutano wa siku mbili jijini Addis Ababa wamepitisha azimio linalotambua utumwa, uhamisho wa kulazimishwa na ukoloni kama mauaji ya kimbari pamoja na uhalifu dhidi ya watu wa Afrika.

Katika hotuba yake, Mwenyekiti Mahmoud Ali Youssouf alisisitiza pia haja ya kusitishwa kwa kile alichokiita kuangamizwa kwa watu wa Palestina, akieleza mshikamano wa bara la Afrika na taifa hilo.

Kwa mujibu wa tamko la mkutano huo, wakuu wa nchi na serikali walikubaliana kuitambua tarehe 30 Novemba kama Siku ya Afrika ya Kuwakumbuka Mashujaa na Waathiriwa wa Biashara ya Watumwa ya Atlantiki, Ukoloni na Ubaguzi wa Rangi (Apartheid).

Aidha, nchi wanachama zilisema zitaendelea kufuatilia suala hilo na kushirikiana ili kuhakikisha azimio hilo linapata utambuzi katika ngazi ya kimataifa.

Chanzo: Africanews

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#