RSF ilifanya mashambulio katika Hospitali ya Al Mazmoum katika jimbo la kusini mashariki la Sennar, taarifa kutoka kwa Mtandao wa Madaktari wa Sudan zimesema.

RSF yashambulia hospitali Sudan, na kuwaua watu kadhaa

Mashambulizi ya ndege isiokuwa na rubani ya wapiganaji wa RSF yamewaua watu watatu na kuwajeruhi wengine saba katika Hospitali ya Al Mazmoum katika jimbo la kusini mashariki la Sennar siku ya Jumapili, Mtandao wa Madaktari wa Sudan umesema siku ya Jumatatu.

Kundi hilo la madaktari limesema katika taarifa kuwa ndege hiyo isiokuwa na rubani ya RSF ililenga hospitali Jumapili jioni, na kuwaua watu watatu na kuwajeruhi wengine saba, ikiwemo mhudumu wa afya.

“Kushambulia vituo vya afya ni ukiukwaji wa wazi sheria za kimataifa ambazo zinapinga kushambuliwa kwa vituo na wahudumu wa afya,” shirika hilo liliongeza.

Matukio kama haya “yanaongeza madhila kwa raia na kuwanyima wakazi nafasi ya kupata huduma za afya,” mtandao huo ulisema, na kuutaja uhongozi wa RSF “kuhusika kwa hilo” la kushambilia hospitali.

Wapiganaji wa RSF hawakutoa taarifa kuhusu tukio hilo.

Mamlaka za nchini Sudan na mashirika ya haki za binadamu yameshtumu RSF kwa kuwalenga raia. Wapiganaji hao hawajajibu hadharani kuhusu shutuma hizo lakini wanasema “wanajitahidi kuwalinda raia.”

Shirika la Afya Duniani (WHO) lilionya Februari 10 kuwa mfumo wa afya wa Sudan uko hatarini baada ya vituo vitatu kushambuliwa katika jimbo la Kordofan Kusini katika wiki ya kwanza ya mwezi.

Mapigano makali yameibuka katika majimbo matatu ya Kordofan — Kaskazini, Magharibi, na Kusini — tangu Oktoba 2025 huku vita vikiendelea katika ya jeshi la Sudan na RSF.

RSF imekuwa ikikabiliana na jeshi la Sudan tangu Aprili 2023 kutokana na kutoelewana kuhusu kuunganisha vikosi hivyo viwili. Mapiganao haya yamesababisha baa baya kabisa la njaa duniani, kuwaua maelfu ya watu, na wengine milioni 13 kulazimishwa kuondoka katika makazi yao.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#