Dollar

43,5385

0.04 %

Euro

51,5119

0.2 %

Gram Gold

6.888,5900

-0.31 %

Quarter Gold

12.309,5300

0 %

Silver

112,3100

-8.28 %

Afrika inakabiliwa na changamoto za kipekee zinazoathiri wagonjwa wa saratani ikiwemo ugunduzi wa kuchelewa na ukosefu wa vifaa wa tiba vya kutosha.

Vifo 4 kati ya 10 vya Saratani barani Afrika vinaweza kuzuiwa kutokana na ugunduzi wa mapema: WHO

Shirika la Afya Duniani WHO, limetoa hofu juu ya kuongezeka kwa janga la saratani barani Afrika, likitaja utambuzi wa kuchelewa, upatikanaji mdogo wa matibabu na hatari zinazoweza kuzuilika ambazo zinaendelea kuendesha ugonjwa huo katika bara zima.

Katika taarifa yake ya kuadhimisha Siku ya Saratani Duniani, Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika, Dk Mohamed Janabi alisema Kuzuia saratani kabla ya kuanza na kuigundua mapema kunaokoa maisha, inaashiria tofauti kubwa ya uwezo wa utambuzi na matibabu kati ya nchi zenye kipato cha juu na nyingi barani Afrika.

‘’Kila mwaka, zaidi ya wagonjwa wapya milioni 1 hugunduliwa, na karibu watu milioni 1 hupoteza maisha kutokana na ugonjwa huo. Nyuma ya idadi hiyo ni akina mama, baba, watoto na vijana ambao maisha yao yamekatizwa si kwa sababu suluhu hazipo, bali ni kwa sababu upatikanaji wa suluhu hizo unabaki bila usawa,’’ Dk Janabi alisema katika taarifa yake.

Alisisitiza kuwa hadi wagonjwa wanne kati ya kila kumi wa saratani duniani wanaweza kuzuilika kwa kushughulikia mambo muhimu ya hatari kama vile utumiaji wa tumbaku, unywaji pombe hatari, ulaji usiofaa, kutofanya mazoezi ya mwili, uchafuzi wa hewa na baadhi ya maambukizo ikiwa ni pamoja na virusi vya human papilloma (HPV) na virusi vya homa ya ini.

WHO ilisema zaidi kwamba takriban asilimia 37 ya visa vipya vya saratani takriban milioni 7.1 duniani mwaka 2022 vilihusishwa na visababishi vinavyoweza kuzuilika.

Onyo kali kutoka kwa ofisi ya kanda linaonyesha kuwa kufikia mwaka 2030 Afrika inaweza kukabiliwa na takriban visa vipya vya saratani milioni 1.6 na vifo milioni 1.2 kila mwaka ikiwa hali ya sasa itaendelea.

Kulingana na utafiti, mwelekeo wa Saratani hutofautiana kulingana na kanda. Kwa mfano, katika Afrika Mashariki, saratani ya shingo ya kizazi, saratani ya matiti na saratani ya kibofu ni kati ya magonjwa mapya ya juu.

Lakini Afrika inakabiliwa na vikwazo vya kipekee vinavyojumuisha matokeo ya saratani.

Uchunguzi wa kuchelewa ambapo wagonjwa wengi huonyesha dalili wakiwa tayari katika awamu ya juu kutokana na ukosefu wa ufahamu na miundombinu ndogo ya uchunguzi, kupunguza uwezekano wa matibabu ya mafanikio.

Nyingine ni Upatikanaji mdogo wa matibabu na sajili dhaifu za saratani na kutoripoti.

Lakini kulingana na Dk Janabi, mwaka uliopita umeonyesha kile kinachowezekana wakati udhibiti wa saratani unapokuwa kipaumbele cha kitaifa.

‘’Nchi katika Mkoa mzima zimepanua chanjo ya HPV, kuimarisha huduma za uchunguzi wa saratani ya mlango wa kizazi, kuboresha upatikanaji wa huduma za saratani kwa watoto, na kuanza kujumuisha huduma matibabu katika huduma za afya za kawaida. Hii ni misingi muhimu ya mafanikio ya muda mrefu ya kuishi.’’

Na WHO inakariri kwamba Saratani sio tena janga la kimya barani Afrika. Ni dharura ya afya ya umma inayoongezeka ambayo inadai hatua za haraka, za usawa na endelevu.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#