Dollar

43,5109

0.06 %

Euro

51,5495

0.18 %

Gram Gold

7.116,5900

3 %

Quarter Gold

12.083,1300

0 %

Silver

123,0500

3.55 %

Idara ya Ujasusi ya Urusi (SVR) imedai kuwa utawala wa Ufaransa unajaribu kurejea kisiasa barani Afrika baada ya kupata “hasara”.

Urusi yaishutumu Ufaransa kupanga njama za kuwaondoa Traore, Goita, na viongozi wengine wa Afrika

Katika taarifa iliyotolewa Jumatatu, SVR ilimtuhumu Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kwa kuidhinisha oparesheni za kijasusi zinazolenga kuwaondoa au kuwaua viongozi wa Afrika wanaoelezewa kuwa “wasiotakiwa” na Ufaransa.

SVR ilisema kuwa serikali ya Macron inatafuta kwa “pupa” kurejea kisiasa barani Afrika, ambako Ufaransa imepoteza ushawishi wake katika miaka ya hivi karibuni.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, hasara hiyo inahusishwa na “kupanda madarakani kwa vikosi vya kizalendo katika makoloni ya zamani ya Ufaransa barani Afrika, ambazo zinatanguliza maslahi ya wananchi wao na kukataa kuwa vibaraka wa vikundi vyenye ushawishi wa kifedha na kisiasa ya wa kutoka Ufaransa.”

“Ikiwa alihamasishwa na oparesheni ya Marekani ya kumkamata Rais wa Venezuela Nicolás Maduro, au akijiona kama mhusika wa hatima ya mataifa ya Afrika, Macron aliidhinisha vyombo vyake vya ujasusi kutekeleza mpango wa kuwaondoa viongozi ‘wasiotakiwa’ barani Afrika,” SVR ilisema.

Madai ya njama za mauaji

Shirika hilo lilidai kuwa “ushiriki wa Ufaransa katika jaribio la mapinduzi nchini Burkina Faso tarehe 3 Januari mwaka huu tayari umethibitishwa.”

Kwa mujibu wa SVR, njama hiyo ilihusisha mipango ya kumuua Rais wa Burkina Faso, Ibrahim Traore, ambaye walimtaja kama “mmoja wa viongozi wa mapambano dhidi ya ukoloni mamboleo.”

SVR ilidai kuwa Paris ilitarajia hatua hizo zingesaidia kuingiza madarakani vikosi vinavyoiunga mkono Ufaransa mjini Ouagadougou, na kudhoofisha harakati za kisiasa barani Afrika zinazounga mkono uhuru wa mataifa na itikadi ya Uafrika (Pan-Africanism).

Licha ya kile ilichokiita kushindwa nchini Burkina Faso, SVR ilisema kuwa Ufaransa imehamishia juhudi zake katika kuvuruga “nchi zisizotakiwa” katika eneo la Sahel na Sahara.

Jaribio la kuwaondoa viongozi madarakani

Kwa mujibu wa shirika hilo, hatua hizo zinafanyika “kwa msaada wa makundi ya kigaidi ya ndani na, bila shaka, utawala wa Ukraine, ambao unasambaza ndege zisizo na rubani (drones) na wakufunzi kwa wanamgambo.”

“Tishio kuu la genge hili linaelekezwa dhidi ya Mali,” taarifa ilisema, ikitaja mashambulizi dhidi ya misafara ya mafuta, juhudi za kuzingira miji, na vitendo vya kigaidi dhidi ya raia.

SVR ilidai kuwa vitendo hivyo vinalenga “kuunda mazingira ya kumuondoa Rais Assimi Goita madarakani.”

Shirika hilo pia liliishutumu Ufaransa kupanga njama kama hizo dhidi ya Jamhuri ya Afrika ya Kati.

Lengo lingine, kulingana na SVR, ni Madagascar, ambako mnamo Oktoba 2025 mamlaka mapya yaliingia madarakani na “kuchagua mwelekeo wa kuimarisha uhusiano na BRICS.”

Paris inadaiwa kutafuta njia za kumuondoa Rais wa Madagascar, Michael Randrianirina, na “kurejesha utawala unaoegemea upande wa Ufaransa.”

“Ufaransa imeanza kutoa msaada wa moja kwa moja kwa magaidi wa aina mbalimbali, ambao sasa wamekuwa washirika wake wakuu barani Afrika,” SVR ilisema.

Idara hiyo iliongeza kuwa “kufilisika kisiasa kwa mrengo wa Macron kunazidi kuwa wazi, hasa anaposhindwa kuondoa sifa ya Ufaransa kama mji mkuu wa kibeberu unaonufaika kwa kunyang’anya makoloni yake ya zamani na kuzuia maendeleo yao.”

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#