Dollar

41,3687

0.09 %

Euro

48,5985

-0.05 %

Gram Gold

4.849,5600

0.44 %

Quarter Gold

0,0000

%

Silver

0,0000

%

Mapigano, maradhi ya kipindupindu, na kupunguzwa kwa ufadhili imeongeza ukali wa janga hilo, asema mwakilishi wa shirikia la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) nchini humo.

UN yaonya ya kwamba mafuriko makubwa Sudan Kusini yanaweza kuathiri zaidi ya watu milioni 1

Mafuriko nchini Sudan Kusini tayari yameathiri watu wapatao 273,000 mwaka huu, na huenda yakaathiri zaidi ya watu milioni 1 katika miezi ijayo, limesema Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) siku ya Ijumaa.

“Sudan Kusini inakumbwa tena na mafuriko makubwa sana, na kwa bahati mbaya, hasa katika maeneo ambayo tayari yameathiriwa na mapigano mapya katika kipindi cha miezi sita iliyopita,” alisema Marie-Helene Verney, mwakilishi wa UNHCR nchini Sudan Kusini, katika mkutano na waandishi wa habari wa Umoja wa Mataifa mjini Geneva.

Verney alisema idadi ya watu walioathirika imeongezeka mara tatu zaidi ndani ya mwezi Agosti pekee, huku takribani watu 100,000 wakilazimika kuhama makazi yao.

“Ikiwa hali hii itaendelea, tunakadiria kuwa zaidi ya watu milioni moja wataathirika katika miezi michache ijayo, ambapo takriban 400,000 watahamishwa,” alisisitiza, akiongeza kuwa mvua za mwaka huu ni kubwa kuliko zile za mwaka uliopita.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#