Dollar

40,9411

0.09 %

Euro

47,9607

0.44 %

Gram Gold

4.383,8900

0.13 %

Quarter Gold

0,0000

%

Silver

0,0000

%

Umoja wa Afrika umeunga mkono kampeni inayolenga kukomesha matumizi ya ramani ya dunia ya karne ya 16 ya Mercator, inayotumiwa na serikali na mashirika ya kimataifa, na badala yake kutumia ramani inayowakilisha kwa usahihi zaidi ukubwa wa Afrika.

Umoja wa Afrika wataka ulimwengu kutumia ramani ya dunia inayoonyesha ukubwa halisi wa Afrika

Ramani hiyo ilibuniwa na mchoraji ramani Gerardus Mercator kwa ajili ya uongozaji, lakini mchoro wake unachanganya kwa kupotosha ukubwa wa mabara: huongeza ukubwa wa maeneo karibu na ncha za dunia kama vile Amerika Kaskazini na Greenland, huku ikipunguza ukubwa wa Afrika na Amerika Kusini.

"Inaweza kuonekana kuwa ni ramani tu, lakini kiuhalisia, sivyo," naibu mwenyekiti wa Kamisheni ya AU Selma Malika Haddadi aliambia Reuters, akisema Mercator ilikuza fikra potofu kwamba Afrika "ilikuwa "pembezoni", licha ya kuwa bara la pili kwa ukubwa duniani kwa eneo, likiwa na mataifa 54 na zaidi ya watu bilioni moja.

Fikra kama hizo zinaathiri vyombo vya habari, elimu na sera, alisema.

Ukosoaji wa ramani ya Mercator si jambo geni, lakini kampeni ya 'Sahihisha Ramani' (Correct the Map) inayoongozwa na vikundi vya utetezi vya Africa ‘No Filter and Speak Up' Africa’ imefufua mjadala huo, na kuyataka mashirika kupitisha makadirio ya 2018 ya Equal Earth, ambayo yanajaribu kuakisi ukubwa wa kweli wa nchi.

"Ukubwa wa sasa wa ramani ya Afrika si sahihi," Moky Makura, mkurugenzi mtendaji wa Africa No Filter, alisema.

"Ndiyo kampeni ndefu zaidi ya habari potofu na lazima ikome." Fara Ndiaye, mwanzilishi mwenza wa Speak Up Africa, alisema Mercator iliathiri utambulisho na fahari ya Waafrika, hasa watoto ambao wanaweza kukutana nayo shuleni.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#