Serikali ya kikoloni ya Uingereza ilipatikana na hatia ya kuwaua wachimba migodi wa Mkaa wa Iva Valley jimbo la Enugu wakati wakiandamana kupinga mazingira mabaya ya kazi.

Uingereza yaagizwa kuwalipa fidia dola milioni $572 wachimba migodi wa Nigeria waliouawa 1949

Mahakama nchini Nigeria imeiagiza serikali ya Uingereza kuwalipa fidia ya pauni za Uingereza milioni 20 (dola milioni $27) kila familia ya wachimba migodi ya mkaa 21 waliouawa 1949 na maafisa wa usalama wakati wa utawala wa Kikoloni, kulingana na shirika la habari la serikali.

Hukumu hiyo ya Alhamisi imefikisha mwisho harakati za kulipwa fidia kutokana na mauaji hayo za miongo kadhaa, zinazoaminika nchini Nigeria kama moja ya matukio yaliyohamasisha mapambano ya uhuru miaka 11 baadaye kutoka kwa Uingereza, 1960.

Wachimba migodi hao waliuawa kwenye Mgodi wa Mkaa wa Iva Valley jimbo la kusini mashariki la Enugu walikuwa wanaandamana kupinga mazingira mabaya ya kazi. Walikuwa kwenye mgodi huo wakati polisi wa Ukoloni walipowafyatulia risasi, kuwaua 21 na wengine wengi kujeruhiwa.

Katika hukumu yake, Jaji Anthony Onovo wa Mahakama Kuu ya Enugu imeupata utawala wa Uingereza wa Kikoloni na hatia ya mauaji hayo na kuamuru kuwa serikali ya Uingereza inatakiwa kuomba radhi rasmi kwa familia za waliouawa.

Serikali ya Uingereza haijatoa tamko lolote kuhusu hilo. Uingerea haikuwakilishwa kwenye mchakato mzima wa shauri hilo.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#