Makubaliano hayo ni ya kuimarisha ushirikiano wa ulinzi na kijeshi wa pande mbili, imesema Wizara ya Ulinzi ya Somalia

Somalia na Saudia Arabia zafanya makubaliano ya ushirikiano wa kijeshi

Somalia na Saudi Arabia zimesaini makubaliano ya ushirikiano wa ulinzi na kijeshi, Wizara ya Ulinzi ya Somalia ilitangaza Jumatatu.

Wizara ilisema katika taarifa kuwa makubaliano hayo yataimarisha ushirikiano wa ulinzi na kijeshi kati ya nchi hizo mbili huku yakigusa nyanja mbalimbali za maslahi ya pamoja.

Hati ya Maelewano (MoU) ilisainiwa na Waziri wa Ulinzi wa Somalia Ahmed Moallim Fiqi na mwenzake wa Saudi Arabia, Mwanafalme Khalid bin Salman, jijini Riyadh, mji mkuu wa Saudi.

Ushirikiano wa kimkakati pia unalenga kuboresha utulivu wa kikanda na usalama wa Bahari ya Sham, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya ndani vya Somalia.

Uhusiano wa Somalia na Saudi Arabia umezidi kuwa wa karibu tangu Israel ilipotambua eneo lake linalotaka kujitenga, Somaliland.

Somalia pia inatafuta msaada wa kiufundi wa hali ya juu na vifaa vya kijeshi kutoka kwa nchi marafiki ili kulinda mipaka yake ya ardhini na anga yake.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#