Sport
Dollar
41,2910
0.2 %Euro
48,4340
0.61 %Gram Gold
4.758,6800
1.43 %Quarter Gold
0,0000
%Silver
0,0000
%Mwanamfalme wa Qatar Sheikh Mansour bin Jabr bin Jassim Al Thani anataka kuwekeza dola bilioni 21 nchini DRC, serikali ya nchi hiyo ilitangaza siku ya Jumatano.
Shirika la uwekezaji la Al Mansour Holding linatarajia kuwekeza dola bilioni 21 katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, ambapo Qatar ni mpatanishi kwa lengo la kumaliza vita vya miaka mingi mashariki mwa nchi, serikali ya DRC ilitangaza siku ya Jumatano.
Mwanzilishi wa shirika hili na mmoja wa Wanamfalme Sheikh Mansour bin Jabr bin Jassim Al Thani alifanya ziara mji mkuu wa DRC, Kinshasa siku ya Jumanne ikiwa sehemu ya ziara yake ya bara la Afrika.
Ujumbe wa Qatar uliwasilisha ‘‘mapendekezo" ya kutaka kuwekeza karibu dola bilioni 21 nchini DRC wakati wa mkutano na Waziri Mkuu Judith Suminwa, ofisi yake ilisema katika taarifa.
Uwekezaji huo utakuwa katika sekta mbalimbali, ikiwemo kilimo, fedha, uchimbaji madini, dawa na haidrokaboni, iliongeza.
Kufanya ziara 'ya kibinafsi' DRC
Comments
No comments Yet
Comment