Dollar

41,3302

-0.08 %

Euro

48,5825

-0.01 %

Gram Gold

4.849,0000

0.07 %

Quarter Gold

0,0000

%

Silver

0,0000

%

Mwanariadha wa Kenya Peres Jepchirchir alishinda mbio za marathon za wanawake katika mashindano ya dunia siku ya Jumapili.

Mkenya Peres Jepchirchir ampiku Tigst Assefa wa Ethiopia kupata dhahabu katika mbio za marathon

Peres Jepchirchir wa Kenya alionyesha kasi ya ajabu katika mita 100 za mwisho na kushinda mbio za marathon za wanawake kwenye mashindano ya dunia Jumapili.

Katika fainali pekee ya kikao cha pili cha asubuhi kwenye Uwanja wa Kitaifa nchini Japani, Jepchirchir alimshinda Tigst Assefa wa Ethiopia kwa sekunde mbili tu baada ya pambano kali.

Wawili hao walikuwa bega kwa bega walipokaribia kilomita ya mwisho ya mbio hizo ngumu zilizofanyika katika hali ya joto na unyevunyevu.

Assefa, aliyewahi kushikilia rekodi ya dunia, alijaribu kuongeza kasi alipokuwa akimalizia sehemu ya nyuma ya uwanja.

Bingwa wa Olimpiki

Lakini Jepchirchir alijitahidi na kumpita mpinzani wake wa Ethiopia aliyekuwa akipunguza kasi, na kushinda dhahabu kwa juhudi kubwa.

Jepchirchir, ambaye ni bingwa wa Olimpiki katika uwanja huo huo kwenye Michezo ya Olimpiki ya 2021 iliyocheleweshwa na Covid, alimaliza kwa muda wa saa 2 dakika 24 sekunde 43.

"Haukuwa mpango wangu wa mwisho kukimbia kwa kasi katika mita za mwisho, lakini nilipoona nimebakisha mita 100 kufika mwisho, nilianza kuongeza kasi. Nilipata nguvu za ziada pale," alisema Jepchirchir.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#