Sport
Dollar
41,2910
0.2 %Euro
48,4340
0.61 %Gram Gold
4.758,6800
1.43 %Quarter Gold
0,0000
%Silver
0,0000
%Mwanasiasa huyo, ambaye uteuzi wake wa kugombea Urais kupitia chama cha ACT Wazalendo ulitenguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi nchini humo (INEC), amesema kuwa hana nia ya kurejea kwenye chama chake cha CCM.
Aliyekuwa mgombea Urais kwa tiketi ya chama cha ACT-Wazalendo cha nchini Tanzania, Luhaga Mpina amesema hana mpango wowote wa kurejea kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Akizungumza Septemba 3, jijini Dar es Salaam, Mpina ambaye uteuzi wake wa kugombea Urais kupitia chama cha ACT Wazalendo ulitenguliwa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi nchini humo (INEC), amesema kuwa hana mpango wa kurudi ‘nyumbani’, licha ya ombi lililotolewa na mgombea Urais wa CCM, Emmanuel Nchimbi.
“Nimesikia wakizungumza kule jimboni kwangu, oooh, Mpina rudi CCM, nyumba ipi…nishasema sitorudi CCM, nimeondoka CCM, sitorudi CCM,” alisema mwanasiasa huyo na mbunge wa zamani wa jimbo la Kisesa.
Comments
No comments Yet
Comment