Sport
Dollar
41,8494
0.02 %Euro
48,6744
0.04 %Gram Gold
5.570,5300
0.02 %Quarter Gold
9.360,7700
0 %Silver
69,2400
0.02 %Kikosi maalum cha kijeshi cha CAPSAT, kilitangaza Jumanne kusimamisha utekelezwaji wa Katiba na kuchukua mamlaka baada ya Bunge kumuondoa madarakani Rais Andry Rajoelina.
Kwa mujibu wa mwandishi wa shirika la habari la Anadolu, CAPSAT ilichukua hatua hiyo baada ya Bunge kupitisha azimio la kumuondoa madarakani Rais Rajoelina.
Kikosi cha CAPSAT, kikiongozwa na Kanali Michael Randrianirina, kiliingia katika Ikulu ya Ambohitsorohitra iliyoko katika mji mkuu, Antananarivo, na kutangaza kuchukua uongozi wa nchi.
Kanali Randrianirina alisema: "Kwa kutumia Amri namba 2025-001, tumeamua kusitisha utekelezwaji wa katiba iliyopitishwa Desemba 11, 2010, na kuanzisha mifumo mipya kwa ajili ya mageuzi ya kitaifa."
Aliongeza kuwa: "Kipindi cha mpito kitadumu kwa muda usiozidi miaka miwili. Katika kipindi hiki, kura ya maoni itafanyika ili kuunda katiba mpya, kisha uchaguzi utafanyika kuanzisha taasisi mpya hatua kwa hatua."
Taasisi zilizosimamishwa
Taasisi tano zimesimamishwa kazi, nazo ni: Mahakama ya Katiba ya Juu, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Seneti, Baraza Kuu la Ulinzi wa Haki za Binadamu, na Mahakama ya Juu ya Haki.
Hata hivyo, Bunge la Taifa limesalia kama taasisi pekee inayofanya kazi.
Jeshi lilitangaza kuwa nafasi ya urais sasa itashikiliwa kwa pamoja na maafisa wake wa kijeshi.
Mapema siku hiyo, Rajoelina alivunja bunge kufuatia wiki kadhaa za maandamano dhidi ya serikali kote nchini, akisema ni muhimu kurejesha utulivu na kutoa nafasi kwa vijana. Hata hivyo, bunge lilipiga kura na kupitisha hoja ya kumuondoa rais mahakamani.
Rajoelina asema yuko "mahali salama"
Tangu Septemba 25, Rajoelina amekuwa akikabiliwa na maandamano yanayoongozwa na vijana kutokana na ukosefu mkubwa wa maji na umeme, pamoja na tuhuma za ufisadi, ambayo baadaye yaligeuka kuwa wito wa kujiuzulu kwake.
Machafuko hayo yalisababisha mabadiliko makubwa serikalini, ikiwemo kuvunjwa kwa baraza la mawaziri na uteuzi wa waziri mkuu na viongozi wapya wa usalama.
Mnamo Jumatatu, Rajoelina alisema alikuwa amejificha "mahali salama" baada ya "jaribio la kumuua," huku ripoti zikidai kuwa alihamishiwa Ufaransa kwa ndege ya kijeshi baada ya kufikiwa kwa "makubaliano" na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron.
Macron alikataa kuthibitisha iwapo Rajoelina alihamishiwa na Ufaransa, akisema akiwa nchini Misri kuwa: "Ninachoweza kusema ni kuwa tunatiwa wasiwasi sana na hali hiyo."
Rajoelina aitaja hali hiyo kuwa "jaribio la kupindua serikali kinyume cha sheria"
Mnamo Jumamosi, CAPSAT – kitengo cha kijeshi ambacho kilimsaidia Rajoelina kuingia madarakani kupitia mapinduzi mwaka 2009 – kilitangaza kuunga mkono maandamano ya wana Gen Z.
Jumapili, CAPSAT ilimteua mkuu mpya wa kijeshi, saa chache baada ya Rajoelina kulaani uungwaji wao mkono kwa maandamano hayo akisema ni "jaribio la kupindua serikali kinyume cha sheria."
Comments
No comments Yet
Comment