Takriban watu 300,000 wa Sudan Kusini wameikimbia nchi mwaka 2025, hasa kutokana na kuongezeka kwa migogoro, Tume ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu ilisema Jumatatu.

Mzozo wasukuma nje watu 300,000 kutoka Sudan Kusini mwaka 2025: UN

Takriban watu 300,000 kutoka Sudan Kusini wamekimbia nchi mwaka 2025 pekee, hasa kutokana na mzozo unaozidi kuongezeka, Tume ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa ilisema Jumatatu.

"Mapigano ya silaha yanaendelea kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa tangu kusainiwa kwa makubaliano ya kusitisha uhasama mwaka 2017, huku raia wakiwa wahanga wakuu wa ukiukwaji wa haki za binadamu na kuhama makazi," Umoja wa Mataifa ulisema katika taarifa.

"Wanawake wanaendelea kuathirika kwa kiasi kikubwa, wakibeba mzigo mkubwa zaidi na hatari za kulazimishwa kuhama," taarifa hiyo iliendelea.

Mwenyekiti wa tume hiyo, Yasmin Sooka, aliwasihi viongozi wa Sudan Kusini "wasitangulize maslahi yao binafsi juu ya maslahi ya watu wao."

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#