Dollar

43,3717

0.25 %

Euro

50,9411

0.02 %

Gram Gold

6.846,2700

0.12 %

Quarter Gold

11.353,8700

1.42 %

Silver

136,6200

2.17 %

Akizungumzia tishio kutoka kwa Mkuu wa Majeshi wa nchi hiyo na mtoto wa Rais Yoweri Museveni, Muhoozi Kainerugaba, Wine alisema:“Mimi si mhalifu bali mgombea Urais na sio hatia kugombea dhidi ya baba yake.”

Bobi Wine: Mimi si mhalifu

Kiongozi wa upinzani nchini Uganda, Robert Kyagulanyi maarufu kama Bobi Wine, amesema kuwa yeye si mhalifu, baada ya kukimbilia mafichoni kufuatia matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa wiki iliyopita nchini humo.

Wine, mwenye umri wa miaka 43, anadaiwa kukimbilia kusikojukulikana, baada ya makazi yake kuvamiwa.

Wine, ambaye aliuita uchaguzi wa Alhamisi iliyopita kama “wizi wa waziwazi”,  amesema kuwa ameendelea kuwa mafichoni, akiwa ulinzi na watu wa ‘kawaida sana’.

Akizungumzia tishio kutoka kwa Mkuu wa Majeshi wa nchi hiyo na mtoto wa Rais Yoweri Museveni, Muhoozi Kainerugaba, Wine alisema:

“Mimi si mhalifu bali mgombea Urais na sio hatia kugombea dhidi ya baba yake.”

Siku ya Jumanne, Kainerugaba, alionesha matamanio yake ya kumrithi baba yake, akiweka wazi azma yake ya kuuondoa uhai wa Wine, kupitia ukurasa wa X.

"Tumeua magaidi 22 wa NUP toka wiki iliyopita,” aliandika Kainerugaba.

"Ninaomba wa 23 awe Kabobi.”

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#