Polisi nchini Tanzania wametangaza amri ya kutotoka nje katika mji wa Dar es Salaam kuanzia saa kumi na mbili jioni.
Amri hiyo imetolewa baada ya kuzuka kwa maandamano ya kupinga shughuli za uchaguzi.
Taarifa ya kutotoka nje imetolewa na Inspekta Jenerali wa Polisi Tanzania Camillus Wambura.
Hapo awali shirika linalofuatilia masuala ya huduma za mitandao duniani, Netblocks limeeleza kuwepo kwa kutatizika kwa huduma za mitandao nchini Tanzania siku ya Uchaguzi Mkuu, ikiwa thibitisho la taarifa za kutokuwepo kwa huduma hizo kama ilivyo kawaida.