Sport
Dollar
40,4453
0.07 %Euro
47,5069
-0.11 %Gram Gold
4.444,5700
-0.31 %Quarter Gold
0,0000
%Silver
0,0000
%Wizara ya afya ya Sudan imeripoti maambukizi mapya ya kipindupindu, huku idadi hiyo ikifika 1,307 na vifo 18 vilivyosababishwa na ugonjwa huo ndani ya wiki moja.
Katika taarifa yake Jumanne, wizara hiyo ilisema maambukizi hayo yalirekodiwa katika majimbo 12 kati ya 18 ya Sudan kati ya Julai 12 na 18, na kuongeza jumla ya maambukizi tangu kuanza kwa mlipuko wa Agosti 2024 hadi maambukizo 91,034, pamoja na vifo 2,302 katika majimbo 17.
Idadi kubwa zaidi ya maambukizi wiki jana ilirekodiwa huko Tawila, Darfur Kaskazini, ikiwa na maambukizi 519, ikifuatiwa na maambukizi 236 huko Qeissan, Jimbo la Blue Nile.
Kwa kulinganisha, wizara iliripoti maambukizi 674 vya kipindupindu na vifo 13 wiki iliyotangulia, kati ya Julai 5 na 11.
Kuporomoka kwa miundombinu ya Sudan
Mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu unaoendelea umeenda sambamba na kuporomoka kwa miundombinu ya Sudan kutokana na mapigano kati ya jeshi na kikosi RSF.
Jeshi na RSF wamekuwa wakipigana vita tangu Aprili 2023 ambavyo vimeua zaidi ya watu 20,000 na wengine milioni 14 kuyahama makazi yao, kulingana na makadirio ya Umojwa wa Mataifa na mamlaka za mitaa.
Utafiti kutoka vyuo vikuu vya Marekani, hata hivyo, unakadiria idadi ya vifo kuwa karibu 130,000.
Comments
No comments Yet
Comment