Dollar

40,9402

0.02 %

Euro

47,6608

-0.13 %

Gram Gold

4.397,8300

-0.21 %

Quarter Gold

0,0000

%

Silver

0,0000

%

Watu milioni 600 barani Afrika bado hawana umeme, Guterres aliuambia mkutano wa Tokyo

Mkuu wa UN asema Afrika lazima ifaidike kwanza na madini yake muhimu

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres siku ya Alhamisi alitoa wito wa kuwepo kwa ushirikiano mkubwa wa dunia na Afrika siku ya Alhamisi, akisisitiza kuwa nchi zenye utajiri mkubwa wa madini lazima zifaidike na kwanza.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Tokyo kuhusu maendeleo ya Kimataifa kwa Afrika (TICAD) huko Yokohama, Guterres anasema Afrika ina madini mengi muhimu na inahitaji kuimarisha teknolojia endelevu lakini bado haijaweza kufaidika na madini hayo.

“Lakini nchi ambazo zina madini zinatakiwa kuwa za kwanza kufaidi zaidi, huku zikiongeza thamani duniani,” alisema, kulingana na taarifa kutoka ofisini kwake.

Ikiwa ina idadi ya vijana zaidi, na yenye raslimali za asili nyingi, na ari ya ujasiriamali, "Afrika ina matumaini ya kushamiri," Guterres alisema.

Mkuu wa Umoja wa Mataifa pia alisisitiza kuhusu mabadiliko ya utawala bora duniani, ikiwemo nafasi ya kudumu ya Afrika katika Baraza la Usalama na ushawishi zaidi katika taasisi za kimataifa za fedha.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#