Sera mpya ya usafiri nchini Uganda inalenga kukuza utalii na ushirikiano wa kimataifa.

Mataifa 40 Yapewa Fursa ya Kuingia Uganda Bila Viza

Serikali ya Uganda imetangaza kuwa raia wa mataifa 40 sasa wanaweza kuingia nchini humo bila viza, hatua inayotarajiwa kuongeza utalii na kurahisisha safari za biashara.

Kwa mujibu wa serikali, wageni kutoka nchi hizo wataruhusiwa kukaa hadi miezi mitatu nchini humo bila kuomba viza kabla ya safari.

Hata hivyo, nchi kama United States, European Union na United Kingdom hazijajumuishwa katika orodha ya mataifa yanayoruhusiwa kuingia bila viza.

Serikali ya Uganda imesema mpango huo unaonyesha dhamira ya nchi hiyo ya kuimarisha utalii, biashara na muunganiko wa watu kati ya mataifa mbalimbali.

CHANZO: Newstimehub

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#