Sport
Dollar
40,2632
0.13 %Euro
46,8411
0.22 %Gram Gold
4.311,9800
0.34 %Quarter Gold
0,0000
%Silver
0,0000
%Mamlaka nchini Ethiopia zimewakamata washukiwa 82 wa kundi la kigaidi la Daesh.
Mamlaka za nchini Ethiopia zimewakamata washukiwa 82 wanaoamini kuwa ni wanachama wa kundi la kigaidi la Daesh, shirika la kijasusi la nchi hiyo lilisema siku ya Jumanne.
Shirika la Kitaifa la Ujasusi limesema wale waliokamatwa wanashukiwa kupewa mafunzo katika nchi jirani na kisha kuingia katika maeneo mbalimbali nchini Ethiopia.
Wamekamatwa mjini Addis Ababa na katika kanda za Oromia, Amhara, Somali na Harari.
Mamlaka zinasema baadhi ya wale waliokamatwa wanaaminika kuhusika katika vitendo vya uhalifu ikiwemo ukusanyaji wa taarifa za kijasusi, kutoa fedha na kuandaa mipango.
Shirika hilo la kijasusi linasema jamii za maeneo hayo zilisaidia kutoa taarifa zilosaidia kuwakamata na uchunguzi unaendelea kwa sasa.
Comments
No comments Yet
Comment