Sport
Dollar
43,0383
0.02 %Euro
50,3215
-0.02 %Gram Gold
6.171,2600
-0.74 %Quarter Gold
10.399,3200
0.08 %Silver
108,5400
-3.5 %Rais wa Uturuki ameeleza msimamo wa Uturuki kuwaunga mkono "watu wa Venezuela marafiki katika kupambania mafanikio, amani, na ustawi."
Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan amesema kuwa amemwambia Rais wa Marekani Donald Trump katika mazungumzo kwa njia ya simu kwamba Venezuela haitakiwi kuingizwa katika hali ya kutokuwa na usalama baada ya kumpindua kiongozi wake Nicolas Maduro.
Akizungumza baada ya mkutano wa baraza la mawaziri siku ya Jumatatu, Erdogan alionya kuwa kukiuka uhuru wa nchi na kudharau sheria za kimataifa ni hatari sana na huenda kukasababisha “matatizo makubwa duniani.”
“Uturuki haiungi mkono hatua zozote za ukiukwaji wa sheria ya kimataifa,” Erdogan alisema, akiongeza kuwa Uturuki inajitahidi kufanya kile kilicho bora kwa Uturuki na “taifa la ndugu zetu wa Venezuela.”
Amesema Uturuki inaunga mkono “watu wa Venezuela marafiki katika kupambania mafanikio, amani na ustawi,” akieleza kuwa Maduro na watu wa Venezuela waliwahi kuonesha urafiki kwa Uturuki hapo awali.
Erdogan pia alisisitiza umuhimu wa kuzingatia sheria za utawala za kimataifa.
Uturuki iko "mstari wa mbele" kwa nchi kote duniani ambazo zinatetea haki, uhalali, na sheria ya kimataifa, alisema.
Marekani ilimteka nyara Maduro na mkewe mapema siku ya Jumamosi kutoka nyumbani kwao katika kambi ya kijeshi na kuwaweka kwenye meli ya kivita ya Marekani kwa ajili ya kushtakiwa jijini New York wakiwashtumu kwa kuhusika na njama ya ugaidi wa mihadarati.
Maduro alionekana kwa mara ya kwanza katika mahakama ya Manhattan siku ya Jumatatu, ambapo alikanusha mashtaka yote ya Marekani.
Kuondolewa kwake kunakuja baada ya Marekani kwa miezi kadhaa kupeleka wanajeshi wengi pwani ya karibu na Venezuela na madai ya kulipua maboti yaliyokuwa yakisafirisha dawa za kulevya.
Trump amesisitiza kuwa Marekani itasimamia utawala wa Venezuela kwa muda na kuuza mafuta ya nchi hiyo kwa mataifa mengine.
Comments
No comments Yet
Comment