Kodi mpya na marufuku ya kusafirisha concentrate ya lithium kuimarisha usindikaji wa ndani.

Zimbabwe Yaanzisha Sera Kali ya Madini Kuongeza Uzalishaji wa Ndani

Baada ya kusafirisha shehena ya kwanza ya lithium sulphate, Zimbabwe inaendelea kutekeleza sera kali za kuongeza thamani ya madini yake kabla ya kuyauza nje ya nchi.

Serikali imeweka ushuru wa asilimia 10 kwa usafirishaji wa lithium concentrate, huku ikipanga kupiga marufuku kabisa usafirishaji huo ifikapo Januari 2027.

Aidha, serikali ilisitisha kwa muda usafirishaji wa concentrate Februari 2026 baada ya kugundua kile ilichokiita “matumizi mabaya katika mchakato wa usafirishaji wa madini.”

Sera mpya pia zinahitaji wachimbaji kuwasilisha taarifa za kifedha na kufuata viwango vya kazi, usalama na mazingira kabla ya kuruhusiwa kuendelea na mauzo ya nje.

CHANZO: Newstimehub

#