Sport
Ukraine imesema kuwa zaidi ya raia 1,780 wa Afrika kutoka nchi 36 tofauti wamejiunga na jeshi la Urusi.
Zaidi ya raia 50 wa Ghana wameuawa katika vita vya Ukraine baada ya “kulaghaiwa kujiunga vitani”, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ghana amesema baada ya ziara yake jijini Kyiv, Ukraine ambako mazungumzo yalijikuta katika suala la kuajiriwa kwa raia wenye asili ya Kiafrika.
Ripoti kuhusu watu hao kulaghaiwa kwenda Urusi kwa ahadi za ajira na kuishia vitani nchini Ukraine zimeongezeka katika miezi ya karibuni, hali iliyosababisha mvutano kati ya Urusi na baadhi ya nchi husika.
Mamlaka za Urusi zimekanusha kuajiri raia wa Kiafrika kinyume cha sheria kupigana nchini Ukraine.
“Tulipewa taarifa kuwa raia 272 wa Ghana wanaaminika kushawishiwa kujiunga katika vita tangu mwaka 2022, ambapo inakadiriwa 55 wameuawa na wawili wametekwa kama wafungwa wa vita,” Samuel Okudzeto Ablakwa aliandika kwenye ukarasa wa mtandao wa kijamii wa X mwishoni mwa Alhamisi.
Katika mkutano na waandishi wa habari siku ya Jumanne, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine, Andrii Sybiha, akiwa amesimama pamoja na Ablakwa, alisema zaidi ya Waafrika 1,780 kutoka nchi 36 tofauti “wamjiunga na jeshi la Urusi”.
Chanzo: Newstimehub
Comments
No comments Yet
Comment