Gavana wa jimbo la Adamawa, Adamu Umaru Fintiri amelaani shambulizi hilo huku maafisa wa eneo hilo wakisema shughuli za kutafuta miili zinaendelea.

Watu wasiopungua 25 wauawa katika shambulio linaloshukiwa kutekelezwa na Boko Haram nchini Nigeria

Watu wasiopungua 25 waliuawa katika mashambulizi mawili tofauti ya kigaidi katika jimbo la Adamawa, kaskazini-mashariki mwa Nigeria, shirika la habari la AFP limeripoti likinukuu maafisa wa eneo hilo.

Mashambulizi hayo katika miji ya Madagali na Hong, iliyoko karibu na mpaka wa Cameroon, yalihusishwa na magaidi wa Boko Haram, ambao wamekuwa wakitekeleza mashambulizi katika eneo hilo tangu kundi hilo lilipoanza shughuli zake mwaka 2009.

“Watu wenye bunduki tunaodhani ni Boko Haram waliokuwa kwenye pikipiki nyingi… walivamia soko. Walifyatua risasi na kuuwa watu 21,” afisa mmoja wa serikali ya mtaa wa Madagali aliliambia AFP kuhusu shambulio la Jumanne jioni, kwa sharti la kutotajwa jina.

Wavamizi hao pia walipora soko na kuiba vyakula pamoja na pikipiki, chanzo hicho kilisema.

Chanzo: Newstimehub

 

 

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#