Dollar

40,2628

0.13 %

Euro

46,8224

0.23 %

Gram Gold

4.316,3400

0.45 %

Quarter Gold

0,0000

%

Silver

0,0000

%

Maonesho hayo ya siku sita yanatarajiwa kuleta pamoja sekta ya ulinzi duniani katika maeneo mbalimbali kote jijini.

Uturuki kuwa mwenyeji wa maonesho makubwa ya kimataifa kuhusu ulinzi Istanbul wiki ijayo

Moja ya maonesho makubwa ya masuala ya ulinzi duniani, Maonesho ya Kimataifa ya Ulinzi, yataanza wiki ijayo jijini Istanbul.

Maonesho hayo ya siku sita yataanza Julai 22 na yataandaliwa na Ofisi ya Rais wa Jamhuri ya Uturuki ikishirikiana na Wizara ya Ulinzi ya Uturuki, sekta ya Ulinzi na Wakfu wa Jeshi.

Maonesho hayo ya 17 yatafanyika sanjari katika Kituo cha Maonesho cha Istanbul, Uwanja wa ndege wa Atatürk, Hoteli ya Wow na Atakoy Marina.

Maonesho hayo yataonesha magari ya kivita, magari yenye silaha ya kutumia mbinu vitani, magari ya ardhini yasiyo na dereva, vyombo vya angani, na baharini, mifumo ya silaha, roketi, makombora ya masafa marefu, silaha za kijeshi, michezo ya kijeshi, suluhu za kielektroniki vitani, vifaa vya kuondoa vilipuzi.

Maonesho hayo yanatarajiwa kuhudhuriwa na idadi kubwa ya watu, pamoja na kuwepo kwa hafla kadhaa za kutia saini makubaliano.

Maonesho yaliyopita yalifanyika Julai 2023 jijini Istanbul.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#