Mfanyabiashara wa Tanzania Rostam Aziz amenunua shirika kubwa zaidi la habari Afrika Mashariki, Nation Media Group (NMG), kutoka kwa familia ya Aga Khan, kampuni hiyo iliripoti siku ya Jumanne.

Mtanzania anunua shirika kubwa la habari Afrika Mashariki kutoka kwa Aga Khan

Mfanyabiashara wa Tanzania Rostam Aziz amenunua shirika kubwa zaidi la habari Afrika Mashariki, Nation Media Group (NMG), kutoka kwa familia ya Aga Khan, chombo hicho kilisema siku ya Jumanne.

Mfuko wa Maendeleo ya Kiuchumi wa Aga Khan (AKFED), kupitia kampuni ya NPRT Holdings Africa Limited (NPRT), ulikuwa unamilikia asilimia zaidi ya 54% ya hisa zote za NMG, kufanya AKFED kuwa mwenye hisa nyingi zaidi.

Mfanyabiashara Aziz, 61, kupitia kampuni yake ya Taarifa Limited, amenunua hisa zote za AKFED huko NMG, gazeti la Nation la Kenya limeripoti. Kimsingi yeye ndiye mwenye hisa nyingi zaidi. Rostam Aziz, ambaye ni mfanyabiashara katika sekta ya mawasiliano, vyombo vya habari, kilimo,masuala ya bandari, nishati, madini, na ujenzi.

Chanzo: Newstimetr

 

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#