Sport
Dollar
42,7215
0.04 %Euro
50,2566
0.05 %Gram Gold
5.909,4500
0 %Quarter Gold
9.739,8100
0 %Silver
87,5400
0.13 %Mamlaka za nchini Ureno zimemshtaki mke wa rais wa Guinea-Bissau aliyepinduliwa, ikiwa ni sehemu ya uchunguzi kuhusu madai ya utakatishaji fedha, polisi walisema siku ya Jumanne.
Mamlaka za nchini Ureno zimemshtaki mke wa rais wa Guinea-Bissau aliyepinduliwa, ikiwa ni sehemu ya uchunguzi kuhusu madai ya utakatishaji fedha, polisi walisema siku ya Jumanne.
Dinisia Reis Embalo, mke wa Umaro Sissoco Embalo, aliwasili mjini Lisbon kwa ndege kutoka Guinea-Bissau sawa na abiria mwingine ambaye alikuwa amekamatwa Jumapili, kufuatia kupata taarifa za ndani.
Abiria huyo aliyepatikana na karibu euro milioni tano ($5.9 milioni) taslimu, na alishukiwa kuhusika na utakatishaji fedha, polisi walisema katika taarifa
Mashtaka ya Dinisia Reis Embalo "yalihusishwa" na uchunguzi huo, msemaji wa polisi wa mahakama waliliambia shirika la AFP bila kutoa maelezo zaidi.
Ndege 'ya kijeshi'
Ndege hiyo iliyowabeba wote wawili ilikuwa awali imeorodheshwa kuwa ya kijeshi na ilitarajiwa kuelekea katika mji wa kusini mwa Ureno wa Beja.
Hata hivyo, "baadaye ilibainika kuwa ndege hiyo na inapoelekea ni tofauti", polisi walisema.
Vyombo vya habari vya Ureno vimeripoti kuwa mshukiwa wa kwanza alikuwa mtu wa karibu wa Rais wa Guinea-Bissau aliyepinduliwa Embalo, ambaye alikimbia nchi baada ya jeshi kumuondoa madarakani katika mapinduzi ya Novemba 26.
Shirika la Habari la Umma RTP lilimtaja kama mfanyabiashara Tito Gomes Fernandes.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ureno Paulo Rangel alisema Jumanne alikuwa anawasiliana na mamlaka za nchini Guinea-Bissau kwa lengo la "kurejeshwa kwa utawala wa sheria."
Comments
No comments Yet
Comment