Dollar

41,3051

0.06 %

Euro

48,7951

-0.01 %

Gram Gold

4.834,7100

-0.46 %

Quarter Gold

0,0000

%

Silver

0,0000

%

Wizara hiyo ilisema washukiwa walikamatwa na mapato kutokana na mauzo hayo, yenye thamani ya takriban pauni 194,000 za Misri ($4,000).

Misri yasema bangili ya dhahabu yenye umri wa miaka 3,000 iliibiwa na kuyeyushwa

Bangili ya dhahabu yenye umri wa miaka 3,000 ambayo ilitoweka kwenye jumba la makumbusho la Misri mapema mwezi huu iliibiwa na kuyeyushwa, Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi hiyo ilisema Alhamisi.

Wizara ya Mambo ya Kale na Utalii hapo awali ilikuwa imeripoti kupotea kwa bangili hiyo, ambayo ilikuwa ya Mfalme Amenemope wa Kipindi cha Tatu cha Kati, aliyetawala Misri karibu 1,000 Kabla Kristu.

Kipande hicho, kilichopambwa kwa shanga za umbo la lapis lazuli, kilitoweka kwenye kwenye maabara ya hifadhi mnamo Septemba 9.

Kufuatia wizi huo, kamati maalum iliundwa kwa ajili ya kukagua vielelezo vilivyomo kwenye maabara, na picha za bangili hiyo iliyotoweka zilisambazwa kwenye vitengo vya mambo ya kale katika viwanja vya ndege, bandari na vivuko vya mpaka wa nchi kavu nchini Misri, kuhofiwa kutoroshwa nje ya nchi.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#