Safari za baharini kuelekea Ulaya zachelewa baada ya ongezeko la mvutano wa kijeshi.

Meli za biashara zabadilisha njia kutokana na hatari katika Mlango wa Hormuz

Kutokana na kuongezeka kwa hatari za kiusalama katika Mlango wa Hormuz, mamia ya meli za biashara na mafuta zimelazimika kubadili njia zao na kuzunguka Rasi ya Cape of Good Hope nchini Afrika Kusini ili kuendelea na safari kuelekea Ulaya.

Taarifa za usafirishaji zinaonyesha kuwa zaidi ya meli 200 zimesimamisha safari au kutia nanga karibu na eneo hilo huku nyingine zikichagua kupitia Bahari ya Hindi na pwani ya Afrika Mashariki. Njia hiyo mbadala inaongeza umbali wa safari kwa maelfu ya kilomita na kuchelewesha usafirishaji kwa karibu wiki mbili.

Wakati huo huo, ripoti zimeeleza kuwa baadhi ya meli za mafuta zimeharibika katika eneo la Ghuba, hali inayoongeza wasiwasi kuhusu usalama wa biashara ya dunia pamoja na usambazaji wa nishati kimataifa.

CHANZO: Newstimehub

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#