Ghana imeanza uchunguzi baada ya madai kwamba baadhi ya watengenezaji wanaongeza plastiki kwenye mafuta wakati wa kukaanga chips za ndizi.

Mamlaka Ghana Zachunguza Madai ya Plastiki Katika Chips

Mamlaka ya Chakula na Dawa ya Ghana imesema imeanza kufanya ukaguzi katika masoko pamoja na vipimo vya maabara ili kuchunguza madai ya uchafuzi wa chips za ndizi.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya video kusambaa mitandaoni ikionyesha watengenezaji wakidaiwa kuyeyusha plastiki aina ya Low-Density Polyethylene kwenye mafuta ya kukaangia.

Kwa mujibu wa mamlaka hiyo, matumizi ya plastiki katika mafuta ya moto yanaweza kusababisha kemikali hatari kuingia kwenye chakula na kuhatarisha afya ya walaji.

FDA imeeleza kuwa itatoa matokeo ya uchunguzi huo baada ya vipimo vya maabara kukamilika.

CHANZO: Newstimehub

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#