Marekebisho hayo yamekuja kufuatia malalamiko ya wanasheria wa Israel kuhusu usahihi wa kihistoria katika maudhui ya maonesho.

Makumbusho ya Uingereza Yarekebisha Maonesho, Yaondoa Neno “Palestina”

 

Makumbusho moja nchini Uingereza imefanya mabadiliko katika maonesho yake yanayohusu historia ya kale ya Mashariki ya Kati kwa kuondoa matumizi ya neno “Palestina” katika baadhi ya maelezo yaliyoandikwa ukutani.

Hatua hiyo imechukuliwa baada ya kikundi cha wanasheria wa Israel wanaoishi Uingereza kuibua hoja wakidai kuwa kulikuwa na upungufu wa kihistoria katika baadhi ya maandishi na picha zilizokuwa zikiwasilishwa.

Kupitia taarifa yao iliyotolewa Jumamosi, walisema makumbusho hiyo imeanza kupitia upya maudhui yake, wakieleza kuwa matumizi ya neno hilo hayakuwa yanaendana kikamilifu na muktadha wa kihistoria uliolengwa.

Wanasheria hao pia walisisitiza kuwa istilahi hiyo inaweza kupuuzia au kuficha mabadiliko muhimu ya kihistoria yaliyotokea katika eneo hilo kwa vipindi tofauti.

Kwa sasa, makumbusho inaendelea kurekebisha maudhui ya maonesho yake ili kuhakikisha taarifa zinazotolewa zinazingatia usahihi wa kihistoria.

Chanzo: TRT Afrika

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#