Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi lafanya tathmini ya utayari wa majini huku mvutano ukiongezeka kati ya Tehran na Washington.

IRGC ya Iran yafanya mazoezi ya kijeshi Hormuz kabla ya mazungumzo na Marekani

Kikosi cha Walinzi wa Mapinduzi ya Iran (IRGC) kimeanza mazoezi ya kijeshi katika eneo la kimkakati la Hormuz, siku moja kabla ya duru ya mazungumzo na Marekani. Kwa mujibu wa taarifa ya IRGC, zoezi hilo linalenga kupima utayari wa vikosi vya majini na kuangalia mipango ya ulinzi katika ukanda huo muhimu.

Hormuz ni moja ya njia nyeti zaidi za usafirishaji wa mafuta duniani, ikiunganisha Ghuba ya Uajemi na Bahari ya Oman. Mazoezi hayo yanaonekana pia kuwa na ujumbe wa kisiasa kwa Washington, wakati mvutano kati ya Iran na Marekani ukiendelea kuongezeka.

Hatua hiyo imekuja baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kutangaza kuwa manowari nyingine ya kijeshi itatumwa katika eneo la Mashariki ya Kati, ishara ya kuongezeka kwa uwepo wa kijeshi wa Marekani katika ukanda huo.

Chanzo: TRT Global

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#