Sport
Dollar
41,4055
0.09 %Euro
48,8997
0.06 %Gram Gold
5.039,9700
1.13 %Quarter Gold
0,0000
%Silver
0,0000
%Barabara kadhaa katika mji mkuu wa Lilongwe, zimefungwa na wafuasi wanaompinga mkuu wa Tume ya Uchauguzi ya Malawi.
Maelfu ya wafuasi wa rais aliye madarakani wa Malawi Lazarus Chakwera ameingia mitaani katika mji mkuu wa Lilongwe, wakipinga matokeo ya awali ya uchaguzi, ambayo mpaka sasa yanaonesha kuwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Arthur Peter Mutharika anaongoza katika matokeo ya awali ya uchaguzi mkuu ulioisha Jumanne wiki iliyopita.
Waandamanaji walifunga barabara kadhaa katika mji huo huku wakiapa kuendelea kuandamana hadi pale “haki itakapopatikana.”
Tume ya Uchaguzi inatarajiwa kutangaza matokeo kabla ya Jumatano kama inavyotakiwa na katiba ya nchi, huku kukiwa na shinikizo la kutangaza matokeo.
“Hali ya ukiukaji”
Hivi karibuni, baadhi ya maafisa waandamizi wa chama wamekuwa wakiwataka wafuasi wao kukataa matokeo, kwa madai kwamba uchaguzi haukuwa wa haki.
Jessie Kabwila, ambae ni katibu wa MCP, ameviambia vyombo vya habari hivi karibuni kuwa chama chake hakiko tayari kukubali matokeo ya uchaguzi kwa sababu ya “ukiukaji mkubwa.”
Comments
No comments Yet
Comment