Dollar

0,0000

%

Euro

0,0000

%

Gram Gold

0,0000

%

Quarter Gold

0,0000

%

Silver

0,0000

%

Kulingana na baraza hilo, uwepo wa ofisi ya ubalozi nchini Vatican, ni wa faida kwa Kenya, kutokana na fursa za maendeleo ya miradi ya kijamii kama vile elimu na dini.

Kenya kuanzisha balozi zake mpya Vatican City, Denmark na Vietnam

Baraza la Mawaziri la Kenya lililoketi Jumanne jioni, limeidhinisha uanzishwaji wa ofisi mpya za ubalozi Vatican City, Denmark na Vietnam.

Katika kikao chake  kilichofanyika Ikulu ya Nairobi, baraza hilo limesema kuwa hatua ya kuanzisha balozi ndani ya Makao makuu ya Kanisa Katoliki duniani, itakuza mahusiano kati ya mataifa hayo matatu.

“Uanzishwaji wa ubalozi wetu huko Vatican utaimarisha uhusiano wetu na taasisi za maendeleo za Kikatoliki ambazo zinaendesha jumla ya shule 7,700 na vituo vya afya 500 nchi nzima,” ilisomeka sehemu ya taarifa ya baraza hilo.

Kulingana na baraza hilo, uwepo wa ofisi ya ubalozi nchini Vatican, ni wa faida kwa Kenya, kutokana na fursa za maendeleo ya miradi ya kijamii kama vile elimu na dini.

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#