Sport
Dollar
39,1461
-0.03 %Euro
44,8230
0.41 %Gram Gold
4.234,1000
0.29 %Quarter Gold
0,0000
%Silver
0,0000
%Katika taarifa kutoka kwa Watawa Wamishenari Wabenediktini, kanisa linasema limelazimika kufunga shughuli katika mkoa huo ambao umegeuka kuwa bonde la kifo.
Kanisa Katoliki limefunga vituo vyake vya wamishenari eneo la Kerio Valley kaunti ya Elgeyo Marakwet nchini Kenya ikiwemo hospitali ya Chesongoch kutokana na hali tete katika eneo hilo.
Katika taarifa kutoka kwa Watawa Wamishenari Wabenediktini, kanisa linasema limelazimika kuzima shughuli katika mkoa huo ambao umegeuka kuwa bonde la kifo.
"Kumekuwa na mvutano mkubwa wa ukosefu wa usalama na kusababisha majeraha ya kiakili na kihisia kwa dada zetu," ilisoma taarifa hiyo na kuongeza kuwa hali hiyo imekuwa ngumu kuendesha huduma muhimu kutokana na ukosefu wa wafanyakazi ambao wanakimbia eneo hilo.
Kanisa hilo ambalo lina takriban wafanyakazi 100, limesema limelazimika kufunga shughuli katika Hospitali ya kanisa la Chesongoch, hatua ambayo inaweza kusababisha maafa kwa mamia ya wakazi wanaotegemea kituo hicho kwa huduma za matibabu.
Kanisa lilibaini kuwa uamuzi ulikuwa umefikiwa ili "kuhakikisha usalama wa watawa wanaofanya kazi katika eneo hilo, wafanyakazi na wale wanaotembelea kanisa kwa huduma tofauti."
Pia ilieleza kuwa hatua hiyo inalenga kuishinikiza serikali kupata suluhu ya kudumu ya amani katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na kuwapokonya silaha raia, na kuwakumbusha watu wa Kerio Valley umuhimu wa kuwepo kwa misheni hiyo kwa jamii.
"Ikiwa jamii haizingatii huduma yetu kama muhimu kwao basi hakuna haja ya uwepo wetu,” iliongeza taarifa hiyo.
Chanzo cha kutokuwa na usalama
Hatua hiyo inajiri siku chache baada ya mauaji ya Padre Cheruiyot Bett na watu wanaoshukiwa kuwa majambazi Mei 22, 2025.
Alipigwa risasi na kuuawa na majambazi katika eneo la Tot la Elgeiyo Marakwet, Kenya, alipokuwa katika kazi yake ya kidini.
Wiki iliyopita serikali ilituma maafisa zaidi wa usalama katika eneo hili ili kulinda shule, hospitali, na miundombinu muhimu katika eneo hilo lenye matatizo la Kerio Valley.
Changamoto ya usalama Kerio Valley inachangiwa na kuenea bila kudhibitiwa kwa bunduki tangu katikati ya miaka ya 1970 wakati shambulio la kwanza lililoathiriwa na bunduki lilitokea eneo la Kaben, linalopakana na Kaunti ya Pokot Magharibi na hivyo kuwa mabadiliko ya dhana katika hali ya migogoro.
Comments
No comments Yet
Comment