Dollar

40,7965

0.11 %

Euro

47,7896

0.35 %

Gram Gold

4.401,1600

0.38 %

Quarter Gold

0,0000

%

Silver

0,0000

%

Afrika Kusini imeielezea ripoti hiyo "kuwa na mapungufu" ambayo Marekani inasema hali ya haki za binadamu Afrika Kusini "imekuwa mbaya" , siku chache baada ya serikali ya Trump kuiwekea ushuru wa asilimia 30 kwa bidhaa zao nyingi wanazouza nje.

Afrika Kusini yaeleza ripoti ya Marekani kuhusu haki kuwa  'siyo sahihi

Afrika Kusini imeitaja ripoti ya Marekani inayozungumza kuhusu hali ya haki za binadamu "kuwa na mapungufu", siku chache baada ya uongozi wa Donald Trump kuiwekea ushuru wa asilima 30 kwa bidhaa nyingi ambazo wanauza nje ya nchi.

Katika ripoti yake ya haki za binadamu ya kila mwaka iliotolewa siku ya Jumanne, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imeishtumu Afrika Kusini kwa kuchukuwa "hatua za kutia hofu katika suala la kuchukuwa ardhi za jamii ya Waafrikaner na ukiukwaji wa haki kwa jamii za walio wachache."

Ikiwa wamewekewa ushuru mkubwa zaidi wa Marekani kuliko nchi yoyote Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Kusini imekuwa ikilengwa na Trump, ambaye ameshtumu sheria za nchi hiyo za ardhi na zile za ajira ambazo ni kwa ajili ya kutatua usawa wa watu wa rangi tofauti.

Wizara ya mambo ya nje ya Afrika Kusini ilijibu siku ya Jumanne ikieleza "kusikitishwa sana" na ripoti hiyo ya Marekani.

'Siyo sahihi na yenye mapungufu'

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#