Sport
Dollar
40,7549
0.07 %Euro
47,7986
0.45 %Gram Gold
4.406,5000
0.5 %Quarter Gold
0,0000
%Silver
0,0000
%Iran ilipiga marufuku ununuzi wa chai kutoka Kenya ikichochewa na madai ya biashara mbovu ya uhalifu iliyohusisha kampuni moja ya Kenya.
Kenya na Iran zimekubaliana kuunda kamati ya pamoja ambayo itafanya kazi ya kuondoa vikwazo vya kibiashara ndani ya siku 60, na hivyo kufungua njia ya kuondolewa kwa marufuku ya mauzo ya chai ya Kenya katika taifa hilo la Mashariki ya Kati.
Makubaliano hayo yalifikiwa wakati wa Kikao cha 7 cha Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Kenya na Iran (JCC) kilichofanyika Nairobi, kikiongozwa na Waziri Mkuu Musalia Mudavadi na Waziri wa Kilimo wa Iran, Dkt. Gholamreza Nouri Ghezalcheh.
Marufuku hiyo ilichochewa na madai ya biashara mbovu ya uhalifu iliyohusisha kampuni moja ya Kenya.
"Kabla ya matukio ya kusikitisha ambayo yalisababisha kusimamishwa kwa mauzo ya chai kwa Jamhuri ya Iran, nchi ilikuwa mojawapo ya waagizaji wakuu wa chai ya Kenya. Mauzo ya chai yaliongezeka kutoka tani 3.2 mwaka 2020 hadi rekodi ya juu ya tani 13 mwaka 2024, na thamani inayolingana ya dola milioni 5 mwaka 2030." alibainisha Waziri Mkuu wa Kenya Mudavadi.
"Ukuaji huu ulifikiwa licha ya bei kikomo ya dola 2 kwa kilo kwa chai ya Kenya ambayo ni ya daraja la juu ikilinganishwa na chai ya India na Sri Lanka iliyofikia dola 4.5 kwa kilo. Serikali ya Kenya inatazamia kuondolewa kwa marufuku hiyo ili uuzaji wa chai ya Kenya hadi Iran urejee," aliongeza Mudavadi.

Comments
No comments Yet
Comment