Sport
Dollar
41,0307
-0.03 %Euro
48,1155
0.6 %Gram Gold
4.511,0500
0.63 %Quarter Gold
0,0000
%Silver
0,0000
%Wakuu hao wa kijeshi walifanya mazungumzo yaliyolenga kutathmini hali ya usalama, mahitaji ya wanajeshi, na mikakati ya kuongeza mashambulizi dhidi ya kundi la kigaidi la Al-Shabaab.
Kamanda wa Jeshi la Somalia, Brigedia Jenerali Sahal Abdullahi Omar, na Mkuu wa kambi ya kijeshi ya Uturuki iliyo nchini humo, inayojulikana kama Kambi ya TURKSOM, Jenerali Sebahattin Kalkan, walifanya ziara ya pamoja ya ukaguzi katika kambi za kijeshi katika eneo la Lower Shabelle — hatua inayoonyesha ushirikiano wa kimkakati kati ya mataifa haya mawili.
Ziara hiyo ililenga "kuongeza juhudi za kuangamiza Al-Shabaab", ambapo wakuu hao wa kijeshi walifika katika eneo la Number 50 na kufanya mkutano muhimu na maafisa wanaoongoza wanajeshi walioko mstari wa mbele.
Mazungumzo yao yalijikita katika kutathmini hali ya kiusalama, kubaini mahitaji ya wanajeshi, na kupanga mikakati ya kuimarisha operesheni dhidi ya kundi hilo la kigaidi.
Al-Shabaab wamekuwa wakisababisha hofu na mashambulizi nchini Somalia kwa zaidi ya miaka 16, wakilenga mara kwa mara vikosi vya usalama, maafisa wa serikali na raia.
Msaada kwa jamii
Comments
No comments Yet
Comment