Video na picha zaonyesha raia wa Colombia wakihusishwa na mafunzo ya kijeshi kwa wapiganaji wa RSF.
Baada ya Umoja wa Mataifa kuweka vikwazo dhidi ya baadhi ya raia wa Colombia, ushahidi wa picha na video umeibuka ukionyesha uwepo wao katika kambi za Rapid Support Forces (RSF) nchini Sudan.
Ripoti zinaeleza kuwa mamluki hao wa Colombia walihusika katika kutoa mafunzo ya kiufundi na kijeshi, ikiwemo matumizi ya droni, uendeshaji wa magari ya kivita, na mbinu za mapigano kwa wapiganaji wa RSF.
Aidha, baadhi ya taarifa zinasema walihusishwa pia na mafunzo kwa watoto walio ndani ya vikosi vya RSF, jambo ambalo limeibua wasiwasi mkubwa katika jamii ya kimataifa.
UN inasema ushiriki wao unaonyesha kiwango kipya cha kimataifa cha kuhusika katika vita vya Sudan vinavyoendelea kwa miaka mitatu.