Sport
Serikali ya Uganda imesema ongezeko la mauzo ya nje limechangia kuimarika kwa uchumi wa taifa hilo.
Katibu wa Hazina wa Uganda, Ramathan Ggoobi, amesema uchumi wa nchi hiyo unaendelea kukua kwa kasi kutokana na utendaji mzuri wa sekta mbalimbali ikiwemo kilimo, viwanda na huduma.
Alisema mafanikio makubwa yameonekana katika mauzo ya nje ambapo mwaka 2025 Uganda ilipata dola za Marekani bilioni 14.4 kupitia biashara ya bidhaa na huduma nje ya nchi.
Kwa mujibu wa Ggoobi, mafanikio hayo yamechangia kuimarika kwa thamani ya shilingi ya Uganda dhidi ya sarafu za kigeni.
Aidha, serikali inalenga kukuza uchumi kwa asilimia kati ya 6.5 hadi 7 katika mwaka huu wa fedha.
CHANZO: Newstimehub
Comments
No comments Yet
Comment