Mashirika ya usalama wa baharini yaonya kuhusu kuongezeka kwa hatari ya makundi ya maharamia eneo la Somali Basin.
Kufuatia kutekwa kwa meli ya mizigo karibu na pwani ya Somalia, mashirika ya usalama wa baharini yameongeza tahadhari kwa meli zinazopita katika ukanda huo kutokana na tishio la maharamia.
Kituo cha Pamoja cha Taarifa za Baharini (JMIC) kimesema kiwango cha tishio katika pwani ya Somalia na eneo la Somali Basin kimepandishwa hadi “kikubwa”, ikimaanisha uwezekano wa mashambulizi ni mkubwa.
Taarifa hiyo imekuja huku ikielezwa kuwa kundi la maharamia linafanya shughuli katika eneo hilo, na meli zote zimetakiwa kupitia kwa tahadhari kubwa huku zikifuata mwongozo wa usalama wa kimataifa.
CHANZO: Newstimehub