Mwanaharakati wa haki za binadamu Boubacar Ould Messaoud ameaga dunia mjini Nouakchott.

Mwanzilishi wa SOS Esclaves Afariki Mauritania

Boubacar Ould Messaoud, ambaye alikuwa mmoja wa wanaharakati maarufu wa kupambana na utumwa nchini Mauritania, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 80.

Messaoud alianzisha shirika la SOS Esclaves mwaka 1995 ambalo lililenga kupigania haki za waliokuwa watumwa na kusaidia kuwajumuisha tena katika jamii.

Kabla ya hapo, alijihusisha na harakati mbalimbali za kisiasa ikiwemo kundi la kupinga utumwa la Al Hor alilolijiunga nalo mwaka 1975.

Mwanaharakati huyo pia aliwahi kutunukiwa Tuzo ya Kimataifa ya Kupinga Utumwa mwaka 2009 kutokana na mchango wake katika mapambano dhidi ya utumwa.

CHANZO: Newstimehub

Comments

Comment

Comment Your email address will not be published. Required fields are marked*

No comments Yet

#